Hujjatul Islam Taqavi, katika Hotuba yake aligusia fursa, changamoto na mikakati ya kukabiliana nazo katika nyanja za elimu, utafiti na utamaduni, na kusisitiza umuhimu wa kupanga kwa umakini na ufanisi.

23 Novemba 2025 - 19:39

Warsha ya Siku 2 kwa Wakuu na Wasimamizi wa Elimu, Utamaduni wa Shule Zinazohusiana na kushirikiana za Tanzania, Malawi, Burundi na Zanzibar yafanyika

Shirika Ia Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt as -ABNA- Jamiat Al-Mustafa (s) - Tanzania, Dar-es-salaam imeandaa warsha ya siku mbili iliyoratibiwa kwa ajili ya wakuu na wasimamizi wa elimu, utamaduni na utafiti wa shule zinazohusiana na zinazosimamiwa katika nchi za Tanzania, Malawi, Burundi na Zanzibar. Warsha hii ilijikita katika masuala ya kielimu, kiutafiti na kitamaduni, ikiwa na lengo la kuboresha ubora wa shughuli za shule husika.

Warsha ya Siku 2 kwa Wakuu na Wasimamizi wa Elimu, Utamaduni wa Shule Zinazohusiana na kushirikiana za Tanzania, Malawi, Burundi na Zanzibar yafanyika

Mwanzoni mwa kikao, Hujjatul-Islam Taqavi alitoa maelezo kuhusu malengo ya msingi ya warsha na kusisitiza mambo yafuatayo:

1_Kutumia ipasavyo uwezo na rasilimali zilizopo katika shule

2_Kukusanya, kuratibu na kusasisha taarifa za elimu, utafiti, utamaduni na Qur’ani

3_Kufanya tathmini ya changamoto za malezi na mafunzo, na kubaini maeneo yenye mapungufu

4_Kuimarisha uratibu na ushirikiano baina ya shule zinazohusiana na zinazosimamiwa katika nchi mbalimbali

5_Kuunganisha, kusawazisha na kuboresha maudhui ya mitaala na masomo

Aidha, aligusia fursa, changamoto na mikakati ya kukabiliana nazo katika nyanja za elimu, utafiti na utamaduni, na kusisitiza umuhimu wa kupanga kwa umakini na ufanisi.

Warsha ya Siku 2 kwa Wakuu na Wasimamizi wa Elimu, Utamaduni wa Shule Zinazohusiana na kushirikiana za Tanzania, Malawi, Burundi na Zanzibar yafanyika

Katika sehemu ya mwisho ya kikao, wakuu wa shule walitoa maoni, mitazamo na uzoefu wao, na wakawasilisha mapendekezo ya vitendo kwa ajili ya kuboresha mchakato wa elimu na shughuli za kitamaduni katika shule zao.

Warsha ya Siku 2 kwa Wakuu na Wasimamizi wa Elimu, Utamaduni wa Shule Zinazohusiana na kushirikiana za Tanzania, Malawi, Burundi na Zanzibar yafanyika

Your Comment

You are replying to: .
captcha